Subscribe:

Ads 468x60px

Pages

Monday, December 23, 2013

MSHINDI WA GARI YA PROMOSHENI YA PAMBIKA NA SAMSUNG APATIKANA.

 Meneja Mauzo na Usambazaji wa Samsung Tanzaia , Sylvester Manyara (kushoto) akimkabidhi funguo mshindi wa gari ya Pambika na Samsung Mitsubishi Double Cabin, Juma Mussa Ramadhani katika promosheni ya Pambika na Samsung iliyomalizika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.Kulia ni msimamizi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid.

 Juma Mussa Ramadhani akifurahia mara baada ya kukabidhiwa funguo



Pambika na Samsung yatangaza mshindi wa Mitsubishi Double Cabin
Promosheni ya msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka ya Pambika na Samsung imefikia tamati Jumatatu baada ya kumshuhudia mshindi wa droo kubwa ya mwisho Bw. Juma Musa Ramadhan (46) ambae ni mfanyabiashara akiibuka mshindi wa jumla wa zawadi kubwa ya gari. Bw. Juma Sasa ndie mmiliki mpya wa gari aina ya Mitsubishi Double Cabin iliyosheheni zawadi kibao toka Samsung ikiwa pamoja na Kompyuta mpakato, Mashine ya kufulia nguo, Jokofu, Galaxy Tab 10.1, jiko la kupashia chakula, Luninga ya LED 32’, deki ya DVD na muziki wa nyumbani.
Akionyesha kutoamini anachokisikia toka upande wa pili wa simu iliyompigia kumtambulisha kuwa mshindi wa Pambika na Samsung, bw. Juma Musa alijawa na furaha yenye mshangao baada ya kupokea simu iliyomtambulisha kuwa yeye ni mshindi wa zawadi ya gari. “Kusema kweli sikuwa nashawishika kabisa kwamba nimeshinda gari jipya aina ya Mitsubishi Double Cabin. Nimejikuta mwenye furaha kupitiliza, ni ngumu kukubali ukweli kwamba nimeshinda gari, sikuwahi kufikiria kitu kama hiki! Nimefurahi sana!,” alisema Bw. Juma mkazi wa Tabata Segerea jijini Dar es salaam.
Droo hiyo ya mwisho iliyofanyika katika eneo la kibiashara la Mlimani City jijini Dar es salaam pia ilishuhudia washindi wengine 15 wakijishindia zawadi mbalimbali toka Samsung katika kufunga pazia la mwisho la promosheni hiyo ambapo tayari imeshawazawadia jumla ya watu 90 toka kuanza kwake.
Pambika na Samsung ilikuwa ni promosheni ya wiki 7 ambayo ilizinduliwa mwanzoni mwa mwezi Novemba ikiwa na lengo kuu la kuwazawadia wateja wa Samsung wanaonunu bidhaa halisi za Samsung na kuzisajili kwenye mfumo maalum wa dhamana. Ujumbe wa kampeni si tu kuwazawadia wateja bali pia kutoa fursa na kuahamsisha Watanzania kuangalia uhalisia na uhalali wa bidhaa wanayonunua kupitia maduka ya Samsung au mawakala waliosajiliwa na Samsung.
Akizungumza mapema na waandishi wa habari, Meneja mauzo na Usambazaji wa Samsung Tanzania, Bw Sylvester Manyara alisema kwamba, “Promosheni hii imekuwa ni safari yenye mafaniko kwa Samsung Tanzania toka kuanza kwake na tungependa kumshukuru kila mmoja kwa kuwa sehemu ya mabadiliko na mafanikio. Promosheni hii imeonyesha ongezeko la 30% la wateja wanaosajili bidhaa zao kwa hiari katika mfumo wetu maalum wa dhamana ya ziada” alisema bw. Manyara.
“Kuonyesha mafanikio, kampeni hii ni moja kati ya mipango ya muda mrefu ya Samsung katika kukabiliana na tatizo la bidhaa feki nchini Tanzania na kuongeza uwelewa juu ya faida za kununua bidhaa halisi. Ni matarajio yetu kwamba huu utamaduni wa kununua bidhaa halisi utaendelea hata mara baada ya kumalizika kwa promosheni ya Pambika na Samsung” aliongezea Bw. Manyara
Pambika na Samsung ilikuwa ni moja ya promosheni kubwa iliyoendeshwa na Samsung Tanzania ambayo ilikuwa ni kampeni ya kitaifa maalum kuwazawadia wateja 15 katika droo za kila wiki katika kipindi cha wiki saba ikifuatiwa na droo kubwa ya kutoa zawadi kubwa ya gari kwa mshindi wa jumla.
 

 Meneja Mauzo na Usambazaji wa Samsung Tanzaia , Sylvester Manyara (kushoto)akimpongeza mshindi wa gari, Juma Mussa Ramadhani mara baada ya kumkabidhi gari yake katika promosheni ya Pambika na Samsung iliyomalizika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Hivi ndivyo Juma Mussa Ramadhani alivyopatikana katika droo hiyo, Hapa akipigiwa simu
 Msindi wa Gari, Juma Mussa Ramadhani (wa pili kulia) alipowasili Mlimani City mara baada ya kupigiwa simu kuwa kashinda gari katika promosheni ya Pambika na Saamsung.
 Juma Mussa Ramadhani akisimulia ilivyokuwa mpaka ameshinda


 Hongera sana

0 maoni:

Post a Comment