Mzee
Yusufu Makamba akishauriana jambo na mwanae January Makamba wkati wa
shughuli za mazishi zikiendelea. Mzee Yusufu Makamba amefiwa na mama
yake mzazi aliyefahamika kama Mariam Masau Kivugo kilichotokea tarehe
21 January 2014.
Mzee
Yusufu Makamba akiwa na mwanae January Makamba wakitafakari jambo baada
ya kupata msiba mkubwa wa kufiwa na Mama mzazi wa Mzee Yusufu Makamba,
Mariam Kivugo.
Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ndugu Abdallah Majura Bulembo akitoa salaam
za pole kwa wafiwa wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Masau Kivugo.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa salaam za pole kwa niaba ya
Chama kwa Mzee Yusufu Makamba na Familia yake wakati wa mazishi ya
Mama wa Mzee Yusufu Makamba.
Mamia
ya watu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Ndugu
January Makamba wakati akitoa salaama za shukrani kwa niaba ya familia
kwa wananchi wote waliojitokeza kwenye mazishi ya Bibi yake Marehemu
Mariam Masau Kivugo yaliofnyika Mehazangulu,Tanga.
Mwili wa Marehemu Mariam Kivugo ukipelekwa msikitini kwa ajili ya kuombewa kabla ya kuelekea makaburini.
Watu wakiwa kwenye nyuso za huzuni wakati wa mazishi ya Bibi Mariam Kivugo ambaye pia ni mama wa Mzee Yusufu Makamba.
:
Katibu
wa NEC itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kuweka udongo kwenye
kaburi la mama wa Mzee Yusuf Makamba aliyefariki tarehe 20 Januari 2014.
WAFANYAKAZI WA KAMAGA FERY WAGOMA KUSHINIKIZA BAADHI YA VIONGOZI KUTOLEWA NA HUDUMA YASIMAMA KWA MASAA KADHAA.
Na Peter Fabian.
G. Sengo blog.
MWANZA.
WATUMISHI wa Kampuni ya Kamanga Fery ya Wilayani
Sengerema leo wameweka mgomo ukishinikiza kuondolewea kwa watumishi wenzao
wawaili na kusimamisha utowaji huduma ya usafiri wa abiria na magari Jijini
hapa.
Hatua hiyo ilielezwa na Mwenyekiti wa Chama cha
wafanyakazi Adamu Yusufu ambaye pia ni Kepteni wa kivuko cha MV Orion cha
Kampuni ya Kamanga Fery Ltd. kinachotoa huduma kati ya Kamanga Wilayani
Sengerema na Kamanga Jijini Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za
kampuni hiyo Mwenyekiti Kapteni Yusufu alisema kwamba wafanyakazi wa kampuni
hiyo kwa ujumla wao wameamua kugoma kutoa huduma ili kushinikiza Mkurugenzi
Wiebke Gaetye kuwaondoa watumishi Renatus Manyanda (Meneja rasilimali watu) na
Anna Malapa (Mhasibu matumizi) kutokana na kuwanyanyasa wafanyakazi wa Kampuni
hiyo.
Mwenyekiti huyo alitaja sababu za mgomo huo kuwa ni
pamoja na Manyanda kuwafukuza watumishi bila kosa, kushindwa kulipa makato ya
mishahara yao kwenye Mfuko wa Jamii (NSSF), kushindwa kulipa mishahara zao kwa
wakati ambapo wanadai tangu mwezi Novemba mwaka jana na kushindwa kufanya
matengenezo ya vivuko vya kampuni hiyo kwa wakati.
“Bila Mkurugenzi kuyashughulikia haya
tunayolalamikia ikiwa ni pamoja na kutuondolea watumishi hawa wanaolalamikiwa
na wenzao, nasi hatuko tayari kufanya kazi na tutaendelea na mgomo hadi kilio
chetu kitakaposikilizwa na kutolewa majibu” alisisitiza.
Kwa upande wa Mhasibu Malapa alisema kwamba amekuwa
akiwanyima malipo yanayoizinishwa na Mkurugenzi ama uongozi wa Kampuni hiyo na
hata amekuwa akitoa kauli za kuwakejeli watumishi wenzake jambo ambalo wamedai
kuchoshwa nalo.
Kufatia mgomo huo uliodumu kwa masaa kadhaa na
kupelekea Mkurugenzi Gaetye kuchukua jukumu la kukaa na wafanyakazi ili
kusikiliza hoja na malalamiko yao ambapo aliamua kumfukuza kazi kwanza Manyanda
kisha kusikiliza malalamiko mengine ili kupoza hasira za wafanyakazi hao.
Akizungumza madai ya wafanyakazi hao Mkurugenzi huyo
alisema kwamba tayari amemfukuza kazi huku hoja za malipo ya mishahara yao
ataifanyia kazi haraka na ile ya NSSF huku Mhasibu Malapa akisimamishwa kwanza
kuchunguzwa na uamuzi wake ukisubili kikao cha uongozi wa Kampuni.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi
(Cotwu) tawi la Kampuni hiyo Kapteni Jorwa Magesa (MV Orion) alisema kwamba
kufatia kikao na Mkurugenzi wao wamelidhika na hatua alizochukua na wamempatia
muda kushughulikia mambo mengine yaliyosalia ikiwa ni malalamiko yao ya msingi.
Hatua ya kuondolewa kwa Manyanda imepongezwa na
wafanyakazi na wananchi wa Kijiji cha Kamanga Wilayani Sengerema ambao juzi
majira ya jioni waliandamana na mabango kumpinga kuendelea kuwa mfanyakazi wa
Kampuni hiyo hali hiyo ilipelekea jana kuwepo mgomo mkali kwa wafanyakazi hao
nao wakipinga kuendelea kuwepo kwa watu hao katika Kampuni hiyo.
Manyanda pia amelalamikiwa na baadhi ya wafanyakazi
waliokataa kutajwa majina yao hadharani kwa madai kuwa Manyanda alikuwa akitumia
pia Jina la Mama Salma Kikwete kumtishia Mkurugenzi huyo raia wa Taifa moja la
Ulaya kuwa akimfukuza naye ataondolewa nchini.
Hadi tunakwenda mitamboni hali ya eneo la Kamanga
fery ilikuwa shwari baada ya Mkurugenzi na wafanyakazi wake kukubaliana
kuendelee kutolewa huduma ya usafiri wa abiria na magari wakati madai yao
mengine yakishughulikiwa na kuchukuliwa hatua za haraka kama walivyokubaliana.
MVUA YATISHIA AMANI MWANZA NA KANDA YA ZIWA KWA UJUMLA
Barabara ya Lumumba jijini Mwanza na heka heka zake katika kipindi cha mvua. |
Mifereji ya maji taka ni finyu nayo ikishinda bila kufanyiwa usafi ikiwa ni pamoja na uzibuaji hali huwa tete. |
Adha waipatayo wafanyabiashara waliopangisha kwenye maduka ya majengo yaliyopo pembezoni kwa kituo cha daladala za Mwaloni zamani karibu na soko kuu. |
Mitaro imejaa, barabara zimejaa maji, Si biashara tena bali sasa ni kila mmoja kuokoa mali zake. |
Chepe chepe...dugu yake tepe tepe. |
0 maoni:
Post a Comment