Subscribe:

Ads 468x60px

Pages

Wednesday, July 15, 2015

KENICE KUKUTANISHA MIKOA SANA KATIKA BONANZA LA POOL NANENANE


Mratibu wa Nanenane Kenice Pool Bonanza 2015 (88 Kenice Pool Bonanza 2015), Michael Machellah(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza rasmi Bonanza hilo litakalofanyika jijini Dar es Saalaa.Katikati ni Meneka wa Kampuni ya KENICE Tanzania, Eustace Masaki na Mwenyekiti wa waamuzi wa mchezo wa Pool Taifa,  Hashimu Shaweji.
 
 
 
 
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya kutengeneza meza za mchezo Pool ya KENICE imetangaza kudhamini Bonanza la mchezo wa Pool utakaoshirikisha Mikoa saba katika kusherehekea Sikukuu ya nanenane lijulikanalo kama “88 Kenice Pool Bonanza 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Kampuni ya Kenice Tanzania Limited, Bwana Eustace John Masaki alisema lengo la kufanya Bonanza hili ni kuendelea kuunga mkono mchezo huu kwa pale ulipofikia  ukizingatia sisi ndio Mabingwa wa kutengeneza Meza zinazotumika katika mchezo huu hivyo tumeona  ni jambo jema na ni sehemu ya pekee ya kukutanisha Vijana ambao ndio wachezaji wakuu wa mchezo huu wakabadilishana mawazo kwa njia ya mchezo wa Pool kuliko kuwaacha wakizagaa vijiweni.
Alisema Masaki, tutambue mchezo wa Pool ni michezo kama michezo mingine na ukizingatia michezo ni furaha,michezo ni afya na michezo ni ajira inayomfanya mtu yeyote kupiga hatua katika maisha ukianzia na sisi kama Kampuni bila wachezaji wa pool huko mitaani, hakuna wa kumuuzia hizi meza za pool tunazozalisha kila siku ambapo itapelekea wafanyakazi tulionao kukosa ajira.Hivyo tunakila sababu za kuunga mkono mchezo huu kuhakikisha unakua na unafaidisha jamii.
Masaki alisema zaidi  jumla ya  Sh.Mil.6 tumetenga kwa ajili ya Bonanza hili katika kusherehekea sikukuu ya nane nane kwa mwaka 2015.
Masaki alizitaja zawadi za Bonanza hilo kuwa Bingwa atajinyakulia Meza ya Pool ya kisasa kutoka Kenice yenye thamani ya Shilingi 2,000 000/= pamoja na pesa taslimu Shilingi 300,000/=
Mshindi wa pili atajinyakulia pesa taslimu Shilingi 500,000/=,mshindi wa tatu 300,000/= na wa nne 100,000/=.
Patakuwa na ushindani wamchezaji  mmoja mmoja (Singles) ambapo Bingwa atajinyakulia zawadi ya pesa taslimu Shilingi 200,000/=,mshindi wa pili 100,000/=,wa tatu 50,000/= na wane 30,000/=.
Nae mratibu wa Bonanza hilo Bwana Michael Machellah alisema  Bonanza hilo litaanza Agosti 7,8 na kumalizika 9,2015 katika Ukumbi wa CCM Mwinjuma Mwananyamala jijini Dar es Salaam kwa kushilikisha vilabu vyote vya mikoa ya kimichezo ya Ilala,Temeke,Kinondoni,Pwani, Morogoro, Iringa na Dodoma.
Machellah alimaliza kwa kutoa wito kwa vilabu vya mchezo wa Pool kujitokeza kwa wingi kuja kushiriki Bonanza hilo la sikukuu ya nanenane.
 

0 maoni:

Post a Comment